Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawatunguKahawatungu
    Button
    • NEWS
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    KahawatunguKahawatungu
    NEWS

    Barobaro Kakamega Achimba Kaburi Na Kupima Jeneza Akitishia Kujiua Kutokana Na Hali Ngumu Ya Maisha

    KahawaTungu ReporterBy KahawaTungu ReporterApril 29, 2019Updated:April 29, 2019No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Email
    [Photo/ COURTESY]
    Share
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Pinterest Email Copy Link

    Wakaazi wa kijiji kimoja mjini Kakamega wameshangazwa na kisa ambacho barobaro mmoja ameamua kujichimbia kaburi mbele ya nyumba yake huku akidai kuwa amechoshwa na maisha.

    Kulingana na mdokezi wetu jamaa huyo kwa jina Fredrick Mumeyu almaarufu Holiday amekuwa akilalama kuwa maisha yamekuwa magumu kutokana na gharama ya maisha kupanda.

    “Maisha imekuwa ngumu, bei ya bidhaa inapanda kila kuchao, kupata kazi imekuwa changamoto kubwa ni heri kujitoa mapema kabla ya gharama kukuwa ghali zaidi,” alisema Mumeyu.

    Kulingana na jamaa zake, barobaro huyo pia amejinunulia jeneza analodai kuwa ni nzuri na linamfaa.

    “Tumekuwa tukisikia tu watu hujichimbia kaburi leo tumeona na macho yetu. Ni jambo la kusikitisha kuona mtu mzima mwenye akili zake akijichimbia kaburi. Hata jana alionekana kwa muhudumu mmoja mjini kakamega akijipima ndani ya jeneza,” alisema mmoja wa wakaazi.

    Read: Mwanaume Ajinyonga Kakamega Baada Ya Kutorokwa Na Mke

    Kulingana na mila na tamaduni za jamii ya Waluhya ni mwiko kwa mtu kufanya kitendo kama hicho na anapaswa kufanyiwa tambiko itakayohusisha kuchinjwa kwa kondoo pamoja na kupewa dawa za kienyeji ili kuondoa laana katika jamii hiyo.

    “Huyu kijana analeta laana kubwa sana kwa familia, itabidi amefanyiwa tambiko itakayohusishwa kuchinja kwa kondoo pamoja na kumtakasa kwa madawa ya kienyeji ili kutoa mazimwi yanayomwandama la si hivyo kuna mtu katika hii jamii hata kama si yeye atajitoa uhai,” alisema Mzee Nicholas, kutoka katika kijiji hicho.

    Inaripotiwa kuwa Holiday anaendelea kulinadhifisha kaburi lake huku wazee wa kijiji wakiwaonya wenyeji dhidi ya kumtisha kutoka kwa kazi yake.

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

    Email your news TIPS to Editor@Kahawatungu.com — this is our only official communication channel

    Kakamega
    Follow on Facebook Follow on X (Twitter)
    Share. Facebook Twitter WhatsApp LinkedIn Telegram Email
    KahawaTungu Reporter
    • Website

    Email: Editor@Kahawatungu.com

    Related Posts

    Businessman dies in tragic stupefying incident in Kirinyaga

    April 6, 2026

    Minor dies after falling from sixth floor of apartment in Eastleigh

    April 6, 2026

    Bouncer fatally strikes man outside a club in Nairobi’s downtown

    April 6, 2026

    Comments are closed.

    Latest Posts

    What Is Conan O’Brien Net Worth?

    April 6, 2026

    Savannah Guthrie Returns to ‘Today’ Show

    April 6, 2026

    Willson Contreras Siblings: All About Willmer and William Contreras

    April 6, 2026

    George Springer Siblings: Meet Nicole and Lena Springer

    April 6, 2026

    Kodai Senga Siblings: Get to Know Kotono Senga

    April 6, 2026

    Sonny Gray Siblings: Meet the Siblings Squad Behind the Baseball Player

    April 6, 2026

    Grant Holmes Siblings: Getting to Know Colby Holmes

    April 6, 2026

    Brett Baty Siblings: Get to Know Jordyn and Lauren Baty

    April 6, 2026
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2026 Kahawatungu.com. Designed by Okii.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.