Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawatunguKahawatungu
    Button
    • NEWS
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    KahawatunguKahawatungu
    NEWS

    IEBC Kununua Masanduku Mengine Mapya Kwa Ajili ya Marudio ya Uchaguzi

    KahawaTungu ReporterBy KahawaTungu ReporterSeptember 22, 2017Updated:September 22, 2017No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Email
    chiloba
    IEBC Chairperson, Ezra Chiloba
    Share
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Pinterest Email Copy Link
    nasa
    IEBC CEO Ezra Chiloba

    Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imetangaza kwamba itanunua masunduku mengine ya kupiga kura kwenye marudio ya uchaguzi wa kiti cha urais unaotarajiwa Oktoba 17, 2017.

    Baada ya majaji wa mahakama ya upeo Jumatano kutoa maelezo kwa undani kufuatia kubatilishwa kwa ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta wa Jubilee wa Agosti 8, wakili wa IEBC Paul Muite aliwasilisha pendekezo kwa Jaji Mkuu David Maraga kura zilizopigwa zitolewe ili masanduku hayo yatumike.

    “Tayari mmetoa uamuzi ambao kwa vyovyote vile hautabadilishwa ila kurejea debeni. Uchaguzi uliopita taifa limegharamika kiasi kikubwa cha pesa, ninaomba kwa heshima zako Jaji Mkuu kura zilizohifadhiwa kwa masanduku zilitolewe ili yatumike kwenye shughuli ijayo,” akaomba Bw Muite kwenye mahakama hiyo jijini Nairobi.

    Akaongeza: “Ikiwezekana kura hizo zihifadhiwe katika mahakama hii kwa sababu za kiusalama.”

    Hata hivyo swala hilo lilipingwa vikali na wakili wa National Super Alliance (Nasa) James Orengo ambaye alipata agizo la mahakama kuhifadhi masanduku hayo kwa miaka mitatu zaidi. “Mheshimiwa Jaji masanduku hayo hayafai kufunguliwa kwa mujibu wa sheria. Yanafaa yasalie yamefungwa kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kwa sababu za kuzirejelea usoni endapo kutakuwa na msukumo,” akaeleza Orengo, ambaye pia ni Seneta wa Siaya.

    Kauli ya Bw Orengo iliungwa mkono kwa dhati na wakili aliyewakilisha Rais Kenyatta na Jubilee Party (JP) Fred Ngatia.

    “Ninaomba ombi la Wakili Muite lifutiliwe mbali. Kura hizo huenda zikatufaa baadaye ikiwamo kuthibitisha aliyeibuka mshindi,” akaeleza Bw Ngatia.

    Hata hivyo Muite alibadilisha ombi lake baada ya kufahamishwa kwamba tume ya IEBC itanunua masanduku mengine. “Nimefahamishwa kuwa IEBC itanunua masanduku mengine. Naomba mahakama itupilie mbali hilo ombi langu,” akasema na kusababisha watu kuangua kicheko mahakamani.

    Muungano wa Nasa ulipinga ushindi wa Rais Kenyatta mahakamani ambapo Jaji Maraga aliagiza IEBC iandae uchaguzi mpya wa urais kwa siku 60.

    Mrengo wa Jubilee umekashifu uamuzi wa mahakama hiyo ukishitumu Maraga kushirikiana na Nasa kuwapokonya ushindi.

    Bw Raila Odinga ndiye kinara mkuu wa Nasa.

    Do you have a story you want told? Do you know of a sensitive story you would like us to get our hands on? Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com

    Email your news TIPS to Editor@Kahawatungu.com — this is our only official communication channel

    Follow on Facebook Follow on X (Twitter)
    Share. Facebook Twitter WhatsApp LinkedIn Telegram Email
    KahawaTungu Reporter
    • Website

    Email: Editor@Kahawatungu.com

    Related Posts

    Murkomen announces security colleges and conservation drive in Kerio Valley 

    December 26, 2025

    Governor Simba Arati under fire over Gusii community spokesman claim

    December 26, 2025

    Two killed in bar fight in Busia

    December 26, 2025

    Comments are closed.

    Latest Posts

    Two killed in suspected Palestinian ramming and knife attack in Israel

    December 27, 2025

    Salah penalty sends 10-man Egypt through at Afcon

    December 27, 2025

    Israel recognizes Somaliland as independent State in historic declaration

    December 27, 2025

    Murkomen announces security colleges and conservation drive in Kerio Valley 

    December 26, 2025

    Jota’s sons to join mascots for Liverpool v Wolves

    December 26, 2025

    US judge blocks detention of British social media campaigner

    December 26, 2025

    Governor Simba Arati under fire over Gusii community spokesman claim

    December 26, 2025

    Former Malaysia PM Najib Razak found guilty in state funds scandal

    December 26, 2025
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2025 Kahawatungu.com. Designed by Okii.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.