Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawatunguKahawatungu
    Button
    • NEWS
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    KahawatunguKahawatungu
    EAST AFRICA

    Indo Solutions Yashutumiwa Baada Ya Kukiuka Mkataba Wa Korosho Na Nchi Ya Tanzania

    Wycliffe NyamasegeBy Wycliffe NyamasegeFebruary 19, 2019Updated:February 19, 2019No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Email
    indo solutions, tanzania
    ACT Wazalendo leader Zitto Kabwe [Photo/Courtesy]
    Share
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Pinterest Email Copy Link

    Kampuni ndogo kutoka Kenya ambayo ilijishindia kandarasi ya kununua korosho kutoka nchi jirani ya Tanzania bado haijafanya malipo yoyote mpaka sasa, hii ni kulingana na Kiongozi wa chama cha Wazalendo Zitto Kabwe Ruyagwa.

    Kabwe Ruyagwa anadai kuwa Indo Power Solutions Ltd ambayo ilitarajiwa kulipa dola milioni mia moja na themanini nuka mbili ($180.2/TZS 400B)haijawasilisha pesa zozote kwa mujibu wa mkataba wa pamoja na LC Magumashi.

    Akizungumza kupitia mtandao wa jamii wa Twitter siku ya Jumanne, Ruyagwa aidha alisema kuwa korosho bado hazijaweza kusafirishwa baada ya mabenki ambayo yalitarajiwa kufadhili shughuli hiyo kugoma.

    “Ile Kampuni ‘hewa’ kutoka Kenya iliyoingia mkataba wa kununua Korosho tani 100K kwa US$180m (TZS 400b) mpaka sasa haijalipa pesa kwa mujibu wa mkataba pamoja na LC magumashi, ” Ruyagwa alisema.

    “Korosho hazijabebwa na mabenki ya ndani yaliyofuatwa kutoa pesa yamegoma. Serikali ya CCM #Maarifaless.”

    https://twitter.com/zittokabwe/status/1097800652196057088

    Aliilaumu Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inayoongozwa na raisi John pombe Magufuli kwa kukosa kutoa mwongozo bora.

    Madhara ya maamuzi fyongo Kuhusu Korosho pamoja na sera za hovyo za Uchumi. Gharama za kuagiza bidhaa kutoka nje ( mafuta, mashine na malighafi) zinakuwa kubwa sana ilhali mauzo yetu nje kiduchu. Serikali ya CCM inatoa kipaumbele kwenye UKATILI dhidi ya Watu,Uchumi chali pic.twitter.com/wdw0Lusefd

    — Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) February 19, 2019

    Kampuni ya Indo Power Solutions ikiwakilishwa na mkurugenzi mtendaji  Brian Mutembei  iliingia katika mkataba wa kununua korosho kutoka kwa wakulima wa nchi ya Tanzania mnamo Januari 30 mwaka huu. Hii ni baada ya kuzipiku kampuni zingine nane zilizokuwa zimeonyesha nia katika biashara ya korosho.

    Licha ya kampuni hiyo kutotambulika hau kuwa na uzoefu wa kununua au kuuza korosho ilipewa kandarasi hiyo.

    Read: Rais Magufuli Atoa Shilingi Milioni 200 Kufadhili Kituo Cha Redio Cha Magic FM, Kinachomilikiwa Na CCM

    Mkurugenzi wa bodi ya nafaka nchini Tanzania Hussein Mansour aliidhinisha mkutaba huo katika makao makuu ya Jumuia ya Afrika mashariki mjini Arusha.

    Vile vile, waziri wa sheria Palamagamba Kabudi, waziri wa biashara Joseph Kakunda na gavana mkuu wa benki kuu ya Tanzania Florens Luoga ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria hafla iyo.

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

    Email your news TIPS to Editor@Kahawatungu.com — this is our only official communication channel

    Chama Cha Mapinduzi Indo Power Solutions Ltd Korosho Raisi John Pombe Magufuli Tanzania
    Follow on Facebook Follow on X (Twitter)
    Share. Facebook Twitter WhatsApp LinkedIn Telegram Email
    Wycliffe Nyamasege

    Email news@localhost

    Related Posts

    Uganda Orders Internet Shutdown Ahead of General Election

    January 13, 2026

    ‘Intended killings’: Tanzania’s election violence ensnared unsuspecting victims

    January 10, 2026

    Five Kenyans including two cops arrested in Tanzania while pursuing a suspect, released

    January 7, 2026

    Comments are closed.

    Latest Posts

    Decomposed bodies found in septic tank in Vihiga

    January 14, 2026

    Two Turks arrested after gun drama with Wajir Governor’s driver in a road rage

    January 14, 2026

    K-pop stars BTS to kick off world tour in April

    January 14, 2026

    Court Stops Suspension of NGAAF CEO Roy Sasaka Telewa

    January 14, 2026

    Man killed and his body dumped in water pan in Kisumu

    January 14, 2026

    Six shot dead in banditry attack on village in Marsabit 

    January 14, 2026

    Wamatangi property near railway line demolished at Nyayo Stadium

    January 14, 2026

    Residents in Tana River Surrender Four More Illegal Firearms to Police

    January 14, 2026
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2026 Kahawatungu.com. Designed by Okii.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.