Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawatunguKahawatungu
    Button
    • NEWS
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    KahawatunguKahawatungu
    EAST AFRICA

    Indo Solutions Yashutumiwa Baada Ya Kukiuka Mkataba Wa Korosho Na Nchi Ya Tanzania

    Wycliffe NyamasegeBy Wycliffe NyamasegeFebruary 19, 2019Updated:February 19, 2019No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Email
    indo solutions, tanzania
    ACT Wazalendo leader Zitto Kabwe [Photo/Courtesy]
    Share
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Pinterest Email Copy Link

    Kampuni ndogo kutoka Kenya ambayo ilijishindia kandarasi ya kununua korosho kutoka nchi jirani ya Tanzania bado haijafanya malipo yoyote mpaka sasa, hii ni kulingana na Kiongozi wa chama cha Wazalendo Zitto Kabwe Ruyagwa.

    Kabwe Ruyagwa anadai kuwa Indo Power Solutions Ltd ambayo ilitarajiwa kulipa dola milioni mia moja na themanini nuka mbili ($180.2/TZS 400B)haijawasilisha pesa zozote kwa mujibu wa mkataba wa pamoja na LC Magumashi.

    Akizungumza kupitia mtandao wa jamii wa Twitter siku ya Jumanne, Ruyagwa aidha alisema kuwa korosho bado hazijaweza kusafirishwa baada ya mabenki ambayo yalitarajiwa kufadhili shughuli hiyo kugoma.

    “Ile Kampuni ‘hewa’ kutoka Kenya iliyoingia mkataba wa kununua Korosho tani 100K kwa US$180m (TZS 400b) mpaka sasa haijalipa pesa kwa mujibu wa mkataba pamoja na LC magumashi, ” Ruyagwa alisema.

    “Korosho hazijabebwa na mabenki ya ndani yaliyofuatwa kutoa pesa yamegoma. Serikali ya CCM #Maarifaless.”

    https://twitter.com/zittokabwe/status/1097800652196057088

    Aliilaumu Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inayoongozwa na raisi John pombe Magufuli kwa kukosa kutoa mwongozo bora.

    Madhara ya maamuzi fyongo Kuhusu Korosho pamoja na sera za hovyo za Uchumi. Gharama za kuagiza bidhaa kutoka nje ( mafuta, mashine na malighafi) zinakuwa kubwa sana ilhali mauzo yetu nje kiduchu. Serikali ya CCM inatoa kipaumbele kwenye UKATILI dhidi ya Watu,Uchumi chali pic.twitter.com/wdw0Lusefd

    — Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) February 19, 2019

    Kampuni ya Indo Power Solutions ikiwakilishwa na mkurugenzi mtendaji  Brian Mutembei  iliingia katika mkataba wa kununua korosho kutoka kwa wakulima wa nchi ya Tanzania mnamo Januari 30 mwaka huu. Hii ni baada ya kuzipiku kampuni zingine nane zilizokuwa zimeonyesha nia katika biashara ya korosho.

    Licha ya kampuni hiyo kutotambulika hau kuwa na uzoefu wa kununua au kuuza korosho ilipewa kandarasi hiyo.

    Read: Rais Magufuli Atoa Shilingi Milioni 200 Kufadhili Kituo Cha Redio Cha Magic FM, Kinachomilikiwa Na CCM

    Mkurugenzi wa bodi ya nafaka nchini Tanzania Hussein Mansour aliidhinisha mkutaba huo katika makao makuu ya Jumuia ya Afrika mashariki mjini Arusha.

    Vile vile, waziri wa sheria Palamagamba Kabudi, waziri wa biashara Joseph Kakunda na gavana mkuu wa benki kuu ya Tanzania Florens Luoga ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria hafla iyo.

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

    Email your news TIPS to Editor@Kahawatungu.com — this is our only official communication channel

    Chama Cha Mapinduzi Indo Power Solutions Ltd Korosho Raisi John Pombe Magufuli Tanzania
    Follow on Facebook Follow on X (Twitter)
    Share. Facebook Twitter WhatsApp LinkedIn Telegram Email
    Wycliffe Nyamasege

    Email news@localhost

    Related Posts

    Three Kenyan youths arrested in Tanzania while headed for Mozambique to join ISIS group

    May 20, 2026

    Ethiopian woman’s joy at rare quintuplets after 12 years trying for a baby

    May 8, 2026

    ACT Wazalendo Rejects Chande Commission Report, Calls for Sweeping Reforms

    May 5, 2026

    Comments are closed.

    Latest Posts

    How to Use Fumitabs

    May 20, 2026

    How to Use FNB eBucks

    May 20, 2026

    How to Use Face Serum

    May 20, 2026

    Two Arrested, Sh4.2 Million Worth of Bhang Seized in Kilifi Anti-Drug Raid

    May 20, 2026

    Kenya Intensifies Ebola Preparedness as Regional Outbreak Raises Alarm

    May 20, 2026

    Three Kenyan youths arrested in Tanzania while headed for Mozambique to join ISIS group

    May 20, 2026

    Man dies in fire incident in Kirinyaga

    May 20, 2026

    Andrea Mitchell Net Worth and Salary

    May 20, 2026
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2026 Kahawatungu.com. Designed by Okii.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.