in

Mwanaume Ajinyonga Kakamega Baada Ya Mke Kumtoroka

Suicide Photo | Courtesy

Biwi la simanzi limeikumba familia moja kutoka kijiji cha Embwambwa eneo  bunge la Lurambi kaunti ya Kakamega baada ya mwili wa mwanaume mmoja  kupatikana ukininginia kwa kamba chumbani mwake.

Patrick Siteti, mwenye umri wa miaka 40, anadaiwa kujinyonga kwa kamba baada ya mkewe kumtoroka huku akimwachia mzigo wa kuwalea wanao.

Kulingana na mamake marehemu Salome Siteti, mwendazake aliamua kuchukua hatua hiyo baada yake kuachwa na mkewe kutokana na hali yao ya ufukara.

Soma: Burundi Yawaachilia Huru Wanafunzi Waliomkejeli Raisi Nkurunziza Kupitia Michoro

Inaripotiwa kuwa jambo hili lilimfanya kusongwa na mawazo, na mara kwa mara amekuwa akijaribu kujitoa uhai kabla yake kuokolewa na jamaa zake.

“Tangia kijana wangu abaki na upweke amekuwa akifanya vitu vya kushangaza, majuma kadhaa kabla ya tukio hili alijifungia kwa nyumba na kuiwasha moto kwa lengo la kujiteketeza lakini akaokolewa na ndugu zake kabla ya moto huo kuenea. Siku chache baadaye alijidunga kisu tumboni tukamkimbiza hospitalini. Amekuwa akisema amechoshwa na maisha na hawezi kuafiki majukumu yake kama baba wa familia,” alisema mamaye mwendazake.

Uchunguzi wa polisi unaendelea.

Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874

Written by KahawaTungu Reporter

Email: Editor@Kahawatungu.com

One Comment

Leave a Reply

Leave a Reply

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

woman torso found in city

Commuters Discover Woman’s Torso Along Landhies Road

Barobaro Kakamega Achimba Kaburi Na Kupima Jeneza Akitishia Kujiua Kutokana Na Hali Ngumu Ya Maisha