Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawatunguKahawatungu
    Button
    • NEWS
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    KahawatunguKahawatungu
    EAST AFRICA

    Wanafunzi Watatu Nchini Burundi Wakabiliwa Na Kifungo Gerezani Kwa Kumchora Rais Nkurunziza Kikejeli

    Francis MuliBy Francis MuliMarch 22, 2019No Comments1 Min Read
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Email
    Mchoro ulioleta utata. [PICHA/ KWA HISANI]
    Share
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Pinterest Email Copy Link

    Wanafunzi watatu wa kike nchini Burundi walitiwa mbaroni wiki iliyopita kwa sababbu ya kumdhalilisha Rais Pierre Nkurunziza kupitia kuichora picha yake kikejeli.

    Kulingana na sheria ya nchi hiyo, wanafunzi hao sasa wanakabiliwa na kifungo cha miaka mitano gerezani kutokana na kosa hilo.

    .Wanagenzi hao watafikishwa mahakamani Jumatatu ijayo kwa kosa la kumkashfu mkuu wa nchi.

    Vyombo vya habari nchini humo vinaripoti kwamba wanafunzi hao walikamatwa na wengine wanne, ambao waliachiliwa baadaye katika hali tatanishi.

    Sio mara ya kwanza nchi hiyo imejipata kwenye kurunzi la kimataifa kwa kuwakamata wanafunzi wanaokejeli kiongozi wa nchi.

    Soma: Samaki Tani 11 Kutoka China Wateketezwa Tanzania Kwa Madai Ya Sumu

    Mnamo mwaka wa 2016, vyombo vya dola nchini humo viliwakamata wanafunzi nane wa shule ya sekondari kwa tuhuma za kumkashfu Rais baada ya kuchora michoro isiyofaa dhidi yake.

    Watetezi wa haki za kibinadamu nchini humo wamekashifu utawala wa Rais Nkurunziza kwa wanachokitaja kuwa unyanyasaji wa haki za wanafunzi wasiokubaliana na uongozi wake.

    Familia za wanafunzi hao zimeelezewa kuwa na hofu kwamba huenda serikali ikawageukia baada ya kuwaweka wanafunzi hao rumande muda huo wote.

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

    Email your news TIPS to Editor@Kahawatungu.com — this is our only official communication channel

    Burundi Pierre Nkurunziza
    Follow on Facebook Follow on X (Twitter)
    Share. Facebook Twitter WhatsApp LinkedIn Telegram Email
    Francis Muli
    • Website
    • Facebook
    • X (Twitter)
    • Instagram
    • LinkedIn

    Follow me on Twitter @francismuli_ Email: Editor@Kahawatungu.com

    Related Posts

    Rwanda closes thousands of evangelical churches

    December 22, 2025

    Tanzania tells non-essential workers to remain home on Independence Day

    December 9, 2025

    Why are they targeted by Tanzanian authorities

    December 5, 2025

    Comments are closed.

    Latest Posts

    Former JOOTHR CEO Dr. George Rae Dies

    December 27, 2025

    Man alleges theft of pistol, Sh570,000 in Machakos

    December 27, 2025

    Man kills girlfriend over missing mobile phone in Naivasha

    December 27, 2025

    AG Oduor Names Panel to Select Waqf Commission Members

    December 27, 2025

    Boy killed, body dumped in estate in Njiru

    December 27, 2025

    Nairobi, Other Regions to Experience Heavy Rainfall in next three Days – Kenya Met

    December 27, 2025

    Jacque Maribe Appeals for Support Following Father’s Passing

    December 27, 2025

    How To Fit A Shower Door

    December 27, 2025
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2025 Kahawatungu.com. Designed by Okii.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.