Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    Facebook X (Twitter) Instagram
    KahawatunguKahawatungu
    Button
    • NEWS
    • BUSINESS
    • KNOW YOUR CELEBRITY
    • POLITICS
    • TECHNOLOGY
    • SPORTS
    • HOW-TO
    • WORLD NEWS
    KahawatunguKahawatungu
    EAST AFRICA

    Samaki Tani 11 Kutoka China Wateketezwa Tanzania Kwa Madai Ya Sumu

    Wycliffe NyamasegeBy Wycliffe NyamasegeMarch 14, 2019Updated:March 14, 2019No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Email
    samaki wateketezwa tanzania
    Share
    Facebook Twitter WhatsApp Telegram Pinterest Email Copy Link

    Shehena ya samaki wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili (TSh 60 milioni) kutoka China wameteketezwa katika dampo la Pugu Kinyamwezi Jijini Dar Es Salaam, Tanzania kwa madai ya kuwa na sumu.

    Samaki hao ambao wanakisiwa kuwa takribani tani kumi na moja waliteketezwa mnamo siku ya Jumatatu baada ya kubainika kuwa wana madini ya Zebaki.

    Kulingana na Mkurugenzi Msaidizi wa Ulinzi Rasilimali za Uvuvi, Nchama Marwa, madini hayo yana madhara kwa jamii na yana uwezo wa kusababisha Saratani na kuharibu uzazi.

    Zoezi hilo lililosimamiwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh.Luhaga Mpina, liliamrishwa baada ya Wizara yake kushinda kesi iliyokuwa imewasilishwa kupinga hatua iyo.

    Wakishuhudia zoezi hilo, wamiliki wa shehena iyo, wameipongeza serikali kwa hatua hiyo na kuziomba taasisi za serikali kushirikiana ili kuwapunguzia hasara waliyoipata.

    Mpaka sasa, vyombo vya habari kutoka nchi ya Tanzania vimebaini kuwa takriban tani 31 wa samaki wanaoingia nchini kutoka China wameteketezwa.

    Inadaiwa kuwa, serikali imekaza kamba katika ukaguzi huo ili kuhakikisha kuwa samaki wanaoingia nchini ni salama kwa binadamu.

    Aidha, serikali imewaomba wanainchi kuripoti visa vya samaki hatari kama hao kwa vituo vya usalama ili kulinda maisha ya binadamu.

    Soma:Tanzania Yabatilisha Sherehe Za Siku Ya Wanawake Duniani, Yavitaka Vyama Pinzani Kujiunga Na Serikali Katika Maadhimisho Rasmi

    Kando na Tanzania, visa vya samaki kutoka China pia vimeripotiwa nchini Kenya huku raisi Uhuru Kenyatta akikashifu hatua ya kuagiza samaki kutoka nje.

    “Jameni tunatoa samaki kutoka China na wenzetu hapa… hata kama finance bill imepita, tunaweza sema hiyo samaki imeingia ni mbaya, kuna njia nyingi serikali inaezafanya kazi ndo tuhakikishe watu wetu wanafaidika,” Raisi Kenyatta alisema.

    Licha ya madai ya raisi, duru za kuaminika zinaarifu kuwa samaki kutoka China ni wengi nchini.

    Email your news TIPS to Editor@kahawatungu.com or WhatsApp +254707482874. You can also find us on Telegram through www.t.me/kahawatungu

    Email your news TIPS to Editor@Kahawatungu.com — this is our only official communication channel

    Samaki Tanzania
    Follow on Facebook Follow on X (Twitter)
    Share. Facebook Twitter WhatsApp LinkedIn Telegram Email
    Wycliffe Nyamasege

    Email news@localhost

    Related Posts

    Man fatally slashes child, injures two others in Kakamega

    April 19, 2026

    Man dies after assault during burial preparations in Nyamira village

    April 19, 2026

    Vocal Kisii UDA MCA Raises Alarm Over Alleged Death Threats

    April 18, 2026

    Comments are closed.

    Latest Posts

    Man fatally slashes child, injures two others in Kakamega

    April 19, 2026

    Man dies after assault during burial preparations in Nyamira village

    April 19, 2026

    Vocal Kisii UDA MCA Raises Alarm Over Alleged Death Threats

    April 18, 2026

    Tinder and Zoom offer ‘proof of humanity’ eye-scans to combat AI

    April 18, 2026

    One dead after car hits pedestrians in Melbourne, police say

    April 18, 2026

    Millions listen to Ethiopian star’s song taking swipe at government

    April 18, 2026

    French film star Nathalie Baye dies aged 77, media report

    April 18, 2026

    Iran closes Hormuz Strait again over US blockade with ships mid-transit

    April 18, 2026
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2026 Kahawatungu.com. Designed by Okii.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.